
Baraza la Magavana limelaumu Wizara ya Afya kwa kuchelewesha utekelezaji wa makubaliano, hali inayodaiwa kuchochea migomo ya wahudumu wa afya.
Mwenyekiti wa Baraza hilo, Ahmed Abdullahi, amesema kaunti zitaanza kulipa madaktari mishahara ya CBA kuanzia Agosti, huku akisisitiza kuwa serikali za kaunti hazina mgogoro na madaktari.
Aidha, amesisitiza kuwa huduma za afya ni jukumu la serikali za kaunti na haziwezi kurejeshwa kwa serikali kuu bila mabadiliko ya Katiba.
