Gavana wa Mombasa, Abdulswamad Shariff Nassir, ameendeleza juhudi za kuhakikisha watoto kutoka familia zisizojiweza wanapata elimu bila vikwazo kwa kulipia ada za shule kwa wanafunzi kadhaa.
Katika hotuba yake, Gavana Abdulswamad alisisitiza kuwa hakuna mtoto anapaswa kukatizwa masomo kwa sababu ya ukosefu wa ada. Aliongeza kuwa serikali ya kaunti itaendelea kusaidia wanafunzi wanaohitaji msaada ili kufanikisha ndoto zao.
