
Wakazi wa eneo la Sabaki mjini Malindi Katika Kaunti ya Kilifi wamefurahia kukumbatia mradi wa kiwanda cha matunda kilichozinduliwa.wakiongozwa na gavana wa Kaunti hiyo Gedion Mung’aro pamoja na wawekezaji mbalimbali.
Gavana wa Kaunti hiyo Gedion Mung’aro amewashukuru washikadau mbalimbali walioshiriki kufanikisha kiwanda hicho , huku amesema kuwa wakulima Katika Kaunti hiyo watanufaika pakubwa.Amesema ukulima ndio uti wa mgongo.Hata hivyo amesema kuwa Lengo Lao kuu nikuhakikisha kuwa watu wanapata kazi. Wakiwemo asilimia themanini ya wamama.
Kulingana na Hussain Fundi ambaye ni mwenyekiti wa wakulima Katika Kaunti ya Tana River amemshukuru gavana pamoja na wawekezaji wengine akiwemo Daktari Godana ambaye ni mwenyekiti wa jumuia ya Pwani kwa kuanzisha mchakato huo mzuri na kuwa tafutia soko kwa inchi za inje.Amesema kuwa wakulima wanayo majukumu makubwa kwa kulisha inchi na hivyo basi wanaposhikwa vizuri wataikuza inchi.Huku amewahimiza wakulima kujiunga na vyama na hata pia kushirikiana pamoja na wageni wanapoletwa ili kukuza uchumi.
